|
MWENYEKITI wa Mtandao wa Asasi za Kiraia Mkoa Lindi (LANGO),
Mudhihiri Mewile, amewataka wakazi wa Somanga kutumia fursa zilizopo za
kutoa maoni ya katiba ili nchi ipate katiba yenye kujali maslahi ya
taifa na si ya wanasiasa.
Akizungumza kwenye mdahalo kuhusu mchakato wa mabadiliko ya katiba
uliofanyika jana kwenye Jimbo la Kilwa Kaskazini, Mawile aliwataka
wananchi kutoogopa kutoa maoni katika katiba mpya, kwani ni mali yao.
Katika mdahalo huo uliofanyika katika maeneo ya Kijiji cha Somanga,
wananchi wengi walijitokeza kutoa maoni ambapo Ally Mohamedi alitaka
katiba ijayo iangalie masilahi ya wazee kwani ndio waliochangia mapato
ya nchi hii.
Husna Seleman alitaka suala la elimu ya vitendo mashuleni kuanzia
shule ya msingi mpaka vyuoni lidhibitiwe na isiwe inafanyiwa mabadiliko
ya mitaala mara kwa mara.
“Kwa upande wangu nilitaka suala la elimu kwa vitendo lianzie katika
shule za msingi hadi vyuoni kwani itasaidia sana, itakapotokea
mwanafunzi ameshindwa mitihani yake ataweza kujiajiri mwenyewe,” alisema
Husna.
|
No comments:
Post a Comment