Saturday, October 20, 2012

‘Maoni ya wananchi ni muhimu katiba mpya’





MWENYEKITI wa Mtandao wa Asasi za Kiraia Mkoa Lindi (LANGO), Mudhihiri Mewile, amewataka wakazi wa Somanga kutumia fursa zilizopo za kutoa maoni ya katiba ili nchi ipate katiba yenye kujali maslahi ya taifa na si ya wanasiasa.
Akizungumza kwenye mdahalo kuhusu mchakato wa mabadiliko ya katiba uliofanyika jana kwenye Jimbo la Kilwa Kaskazini, Mawile aliwataka wananchi kutoogopa kutoa maoni katika katiba mpya, kwani ni mali yao.
Katika mdahalo huo uliofanyika katika maeneo ya Kijiji cha Somanga, wananchi wengi walijitokeza kutoa maoni ambapo Ally Mohamedi alitaka katiba ijayo iangalie masilahi ya wazee kwani ndio waliochangia mapato ya nchi hii.
Husna Seleman alitaka suala la elimu ya vitendo mashuleni kuanzia shule ya msingi mpaka vyuoni lidhibitiwe na isiwe inafanyiwa mabadiliko ya mitaala mara kwa mara.
“Kwa upande wangu nilitaka suala la elimu kwa vitendo lianzie katika shule za msingi hadi vyuoni kwani itasaidia sana, itakapotokea mwanafunzi ameshindwa mitihani yake ataweza kujiajiri mwenyewe,” alisema Husna.

No comments:

Post a Comment