|
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekitaka Chama Cha
Mapinduzi (CCM) na viongozi wake kulivunja Bunge ikiwa kina ujasiri,
uzalendo na uadilifu ili kuwezesha mabadiliko ya mfumo wa utawala.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA,
John Mnyika kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari akielezea kauli ya
CCM iliyotolewa na Katibu wake wa Itikadi na Uenez Nape Nnauye na
kusema inapaswa kuwa katika vitendo zaidi kwa kuwavua uanachama viongozi
waliotuhumiwa kwa ufisadi tangu mwaka 2007.
“CHADEMA kinaukumbusha umma kauli ya Mwalimu Nyerere kwamba chama
legelege, huzaa serikali legelege, matokeo ya hali hiyo ni kuwa Bunge
legelege, hali hii inajidhihirisha kwa CCM kushindwa kushughulikia
tuhuma za ufisadi dhidi ya viongozi wake ndani ya chama, Serikali na
Bunge hali inayoathiri uwezo na uadilifu wa vyombo vya uchunguzi na
kuchukua hatua zinazostahili,” alisema Mnyika.
Alisema CCM imeshindwa kusimamia misingi ya kupambana na rushwa kwa
kutumia wingi wa wabunge wake kupitisha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi
nchini kuwa viongozi wa kamati muhimu za Bunge na kuwataja baadhi yao
kuwa ni Kamati ya Mambo ya nje, Ulinzi na Usalama ambayo mwenyekiti wake
ni Edward Lowassa na Kamati ya Fedha na Uchumi, mwenyekiti wake ni
Andrew Chenge.
Mnyika pia aliutaka umma upuuzie kauli ya CCM ya kulipongeza Bunge kwa
kusimamia rasilimali za nchi na kuhakikisha nchi inapiga hatua
kimaendeleo, badala yake CHADEMA itaanza kuunganisha nguvu ya umma
kutaka kamati zote za Bunge zivunjwe na kuundwa upya ili kuurejesha
mhimili huo kwenye mwelekeo unaostahili.
|
No comments:
Post a Comment